[go: nahoru, domu]

Nenda kwa yaliyomo

Haru Mutasa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
The printable version is no longer supported and may have rendering errors. Please update your browser bookmarks and please use the default browser print function instead.

Haru Mutasa ni mtangazaji wa Al Jazeera ya Kiingereza, afisi ya Nairobi. Al Jazeera ya Kiingereza ni stesheni ya kwanza inayotoa habari kwa lugha ya Kiingereza iliyo na makao yake makuu katika nchi ya Kiarabu.[1][2]

Yeye amewahi kufanya kazi na South African Broadcasting Corporation (SABC), CNN, Television New Zealand (TVNZ), Associated Press Television News (APTN) na Star Sports Network.

Kama ripota mjini Harare, Zimbabwe, Haru aliwahi kuripoti taarifa nyingi kuhusu Zimbabwe zilizoonyeshwa katika kipindi cha Inside Africa (CNN), Television New Zealand (TVNZ) na APTN.

Mwaka wa 2007, Haru aliteuliwa kwa "Young Journalist of the Year" (Mwanahabari Mdogo Zaidi katika Mwaka huo) katika tuzo ya Royal Television Society.

Marejeo

Viungo vya nje