[go: nahoru, domu]

Nguva Quotes

Quotes tagged as "nguva" Showing 1-2 of 2
Enock Maregesi
“Unapokuwa mbali na Mungu unakuwa mbali na mwanga, unakuwa gizani, unakuwa mbali na joto, unakuwa katika baridi ya milele. Unapokuwa katika baridi ya milele rangi ya ngozi yako itabadilika na kuwa bluu. Macho yako yatakuwa makubwa kama ya nguva. Bluu maana yake ni kuwa mbali na maarifa ya Mungu. Nguva maana yake ni kuwa mbali na utukufu wa Mungu. Kuwa karibu na maarifa ya Mungu na utukufu wa Mungu, usiwe mkristo wa kanisa, usiwe mkristo wa dini, kuwa Mkristo wa Yesu Kristo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kwa vile hatasamehewa, Shetani hatawasamehe wanadamu. Atahakikisha anauwa kila mtu duniani na kumpeleka kuzimu; ambako anaishi yeye, majini, malaika waovu, wana wa Mungu waliotumwa na Mungu kuja duniani kufundisha watu utukufu lakini wakaasi na Mungu akawalaani (au Wanefili) pamoja na nguva. Nguva ni uzao wa Wanefili na samaki wa baharini na malaika wauvu na wanapatikana zaidi katika Bahari ya Atlantiki, ambako mkuu wake ni Malkia wa Pwani, na katika Bahari ya Hindi ambako mkuu wake ni Malkia wa Bahari ya Hindi. Chini ya Bahari ya Hindi ndipo yalipo makao makuu ya ufalme wa giza hapa duniani.”
Enock Maregesi

Quantcast